Posts

Showing posts from April, 2017

Historia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi:1

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan,hakika leo ni siku nyingine tunakutana katika ukurasa wetu kama ilivyo ada kujuzana mambo mbalimbali yahusuyo Dini yetu Adhwiim ya UISLAAM,na leo hii kwa Idhin  ALLAH tutaangalia Historia ya Mjumbe wa mwisho wa ALLAH kipenzi cha ALLAH, Kiigizo chema kwetu Mtume Muhammad(S.A.W),naamu twendeni pamoja In Sha Allah. Mtume Muhammad(S.A.W) alizaliwa Makka-Arabuni tareh 12-Rabbil Awwal(Mfungo sita) Miaka 54 BK.Sawa na 20(04) 570/571.B.I,Juma Tatu Alfajiri.Ndugu zangu kwenye swala la mwaka wa kuzaliwa kwake hapa kuna Maulamaa wametofautiana na ndiyo maana nimeweka miaka yoote miwili hapo.                        "Na sema ukweli umefika nauongo umetowekw/utaondoka,kwa hakkika uongo  ni wenye  kuondoka"( QUR'AN.17:81). Baba yake alikuwa akiitwa Abdallah(ikiwa na maana ya mja wa ALLAH) na alifariki miezi 6 kabla ya kuzaliwa kwa mwanae Muhammad,na ...

Nguzo(5) za Uislaam.

Aslaam 'Alaykum Wa Rahmatullah Wa Barakatuh ndugu zangu katikan Iymaan,hakika leo kwa mara nyingine tena kwa uwezo wa Allah(S.W) tunakutana tena kwenye ukurasa wetu kujuzana amma kukumbushana mambo kazaa wa kazaa bi mana kwamba Binadam ni mwenye kughafirika.Kabla ya yote basi tumshukuru Allah(S.W) kwa kutuweka hadi leo hii Sha'aban 2/1438 sawa na 29/4/2017 huku tukiwa tunaukaribia mwezi wa Ramadan.Hivo basi kwa uchache wa shukuran basi tuseme ALHAMDULILLAH na kwa uwingi wake basi ni kutekeleza yale Allah aliyotuamrisha.Leo tutaenda angalia Nguzo tano za Uislam yaani vitu vitano muhimu vinavyofanya Uislaam uitwe hivi bi mana kwamba bila hivi vitu Uislaam hijakamilika, twendeni pamoja kwa Uwezo wa ALLAH. Shahadul Llah, yaani kushuhudia kwa Allah ikiwa na maana kwamba  kutamka shahada yaani (Ashahud Llah ilah ila Allah wa ashahadu anna Muhammad Rassulullah) Maana yake ni kwa nashuhudia hakuna Mwenyezi Mungu apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah na Muhammad ni Mtume wake.,hi...

Hatua (5) za kufanya wakati unamlingania mtu.

Image
 Aslaam Alaykum Wa Rahmatullah Wa Barakatuh ndugu zangu, naam hakika kwa uwezo wa ALLAH leo tunakutana tena na kama ilivyo ada kwa uchache wa shukran tuseme Alhamdulillah ikiwa tunamshukuru "ALLAH MTUKUFU MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU" Leo hii tutaangalia hatua ama vitu(5) vya kufanya wakati wa kumlingania mtu. Naam: KULINGANIA- ni kitendo cha kumueleza mwana wa Adam kuhusu Dini tukufu ya UISLAM na faida zilizopo ndani yake, kwa maana nyingine tunaweza sema ni kumshawishi Mja arejee kwa Mola wake kupitia Dini tukufu ya UISLAAM. Hivyo basi kwa kuwa ALLAH katuleta hapa Duniani kwa lengo kubwa la kulingania Dini yake kama vile walivyofanya Waja wema(Mitume&Manabii) basi nasi tulobakia tuendeleze jukumu hili kwa usahihi wake ikiwa kufuata hizi hatua(5). SALAAM, yaani "Aslaam Alaykum Wa Rahmatullah Wa Barakatuh" hii ni salam ya kiislam ambayo kila aliye muislam anapaswa kumsalim aliye muislam mwenzake na kwa Manaswala(wasio waislam) kama vile il...

Buthula'anul Wudhuu(Yanayotengua Udhu).

Aslaam Alaykum Wa Rahmatullah Wa Barakatuh ndugu zangu katika Imaan, kwanza tumshukuru ALLAH(S.W) kwa kutuchagua kuwa miongoni mwa waja wake wenye kuiona leo hii tukiwa na Afya swafi maana kuna wengi wanaohitaji kuwa kama sisi lakini Allah kawaja'alia Mtihani,tuseme In Sha Allah ALLAH awaja'alie Tawfiq,kwa hiyo tulo wazima basi tumshukuru ALLAH kwa uchache wa shukran kwa kusema ALHAMDULILLAH. Leo Bi Idhin Llah In Sha Allah tutaangalia Mambo(5) ambayo kwamba yanatengua Udhu kwa Mtu na kumfanya asiwe na Rukhsa ya ALLAH kuiendea SWALA.Twendeni pamoja. Ghuruj Shay'in min ahadil sabih layn . ( yaani kutokwa na kitu kwenye moja kati ya njia/tupu mbili) hapa kinachomaanishwa ni kwamba ikiwa mmoja wetu ametokwa na haja kubwa ama ndogo basi Udhu wake utakuwa na mushkiri hadi pale atakapostanji(kutawadha/kujichamba).  Naumi (Naumi ni usingizi hivyo ikiwa mtu amelala kisha akaamka basi yamlazimu kuchukuwa Udhu ili aendelee na Swala na hii ni kwa sababu wakati wa usingizi kuna me...

Mitume 25 iliyotajwa kwenye QUR'AN.

Aslaam Alaykum Wa Rahmatullah Wa Barakatuh.ndugu zangu katika Imaan.Sote tunafaham kuwa kuna Mitume(Wajumbe wa ALLAH) mbali mbali ambao aliwateremsha hapa Duniani kwa lengo la kulingania Dini yake tukufu ya UISLAM na kuwaelekeza waja wake kwenye njia ilo sahihi yaani ilo nyoofu ili wapate faida hapa Duniani na kesho Akhera, Lakini je katika Qu'ran tukufu tunajuwa wangapi wametajwa kuanzia wa kwanza hadi mwisho?Basi leo kwa Idhin ya  ALLAH In Sha Allah tuwafahamu Wajumbe hao wa ALLAH. 1)Adam 2)Idris 3)Nuh 4)Saleh 5)Shuayb 6)Hud 7)Ibrahi m 8)Lut 9)Ismail 10)Is-haq 11)Yaqub 12)Yusuph 13)Yunus 14)Mussa 15)Harun 16)Ayyub 17)Daud 18)Sulayman 19)Ilyas 20)Alyasa 21)Dhul-kifl 22)Zakaria 23)Yahya 24)Issa 25)Muhammad "REHMA NA AMAAN ZIWE JUU YAO" Tukutane siku nyingine kwenye Mada nyingine. "FIKISHA YALIYOFIKISHWA" Wa azah Aslaam Alaykum Wa Rahmatullah Wa Barakatuh.