Posts

Nguzo [5] za Uislam.

Aslaam 'Akaykum warahmatullah wabarakatuh ndugu zangu katika Iymaan naam baada ya mda mrefu pia leo twakutana tena ili kujuzana ama kukumbushana hili na lile kuhusu Dini yetu adhwim ya Uislam Dini ya haki.Kama vile tunavojua kuwa sie waja wa Allah hatujakamilika na ni wenye kusahau hivyo ni jukum la kila mmoja wetu kumkumbusha mwenzake. Na leo hii tutaangalia Nguzo [5] kuu z Uislam ambazo kwamba endapo tukishikamana nazo ki ukweli ukweli wa Moyo basi tutakuwa waislam kamili na Allah ataturidhia na Radhi zake tutaanza kuziona hapa hapa Duniani kabla ya kesho Akhera,Hivyo basi tuanze hapa. Kalmat Tawheed/Shahada           Ina maana kwamba ni kushuhudia kwa Allah peke yake na si viumbe vingine na kuamini kuwa Muhamamad ni Mtume wake .[Ashahad Llah ilaha ila ALLAH wa ashahad anna Muhammad Rassulullah] Ndugu zangu Shahada ndiyo nguzo ya kwanza ya Uislam ndiyo mana inatajwa kwenye kila kitu kinachohusiana na Uislam kama vile kwenye Swala,Dua'a hata mtu an...

Historia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi :7

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan naam baada ya Muda mrefu wa kukaa kimya hakika leo tunaendelea kujuzana na tukiwa mwisho kabisa wa Historia ya Mtume Muhammad(S.A.W),na kabla ya yote niwaombe radhi ndugu zangu maana nakaa kimya kwa mda mwingi lakini In Sha ALLAH Allah ataweka wepesi .Na leo tutaangalia kuanzai  Hija ya Mtume Muhammad(S.A.W) hadi kifo chake ambapo ndiyo mwisho wa Historia yetu, BISMILLAH RAHMAN RAHEEM. HIJA YA KUAGA BAADA YA KURUDI MAKKA. Mtume Muhammad kafanya Hijja yake katika mwaka wa 10 baada ya Hijra(10 B.H) na ijapokuwa toka aanze ujumbe wake haikufika Miaka 24,lakini kulikuwepo Waislamu 114,000 waliofutana naye kwenda Makka.Kwa hakika mwengine aliyepata ushindi  mkubwa kama huuu, kwani tukianza Mika 11 nyuma  tunamuona Mtume  akitolewa Makka na kusakwa kutaka kuuliwa na leo ni kiongozi bor a wa Arab na Dunia ya Waislam kwa ujumla. Khutba ya mwisho aliyoitoa Mtume Muhammad(S.A.W) katika mnasaba huu w...

Histotia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi :6

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan,naam Alhmadulillah kwa kuwa tunakutana tena leo hii kwenye muendelezo wa Historia ya Mtume Muhammad kwa uchache wake na tukiwa mwishoni mwa Mada yetu. BISMILLAH RAHMAN RAHIIM. MAPOKEZI YA MTUME MUHAMMAD NA ABU BAKAR SIDIQ KATIKA JAMII YA MADINA BAADA YA KUWASILI KWAO.  Mtume Muhammad na Abu Bakar walipowasili Madina walipokelewa kwa shangwe na furaha na Waislam wa Madina kwani  walikuwa na hamu kubwa ya kumuona Mtume  wa Mwenyezi Mungu. Mtume Muhammad baada ya kufika Madina alimuachia Ngamia wake (HATAMU) ambae alikuwa anamtumia katika usafiri, na Ngamia huyu alienda kusimama  katika kiwanja tupu cha ndugu wawili Mayatima na kuanza kula majani, na Mtume Muhammad aliamua kununua kiwanja kile na kujenga Msikiti na nyumba ndogo ya pembeni. Baadae Msikiti huu pamoja na nyumba ile vilikuwa sehemu ya kufikia wegeni(wasafiri) wasiokuwa na mahali pa kufikia, pia ilikuwa ni sehemu ya mikutano...

Historia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi :5

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan naam katika mwendelezo wetu kuhusiana na Historia ya Mtume wetu Habeeb Muhammad(S.A.W)leo hi tunakutana tena.Na kabla ya yote basi tumshukuru ALLAH kwa kutupa afya hadi leo hii bi mana kwa kuna wengine wengi ALLAH kawaja'alia Mitihan mbalimbali.basi kwa uchache wa shukran tuseme ALHAMDULILLAH.  Naam na leo hii tutaangalia baada ya Muhammad kutangaza Dini kwa wapinzani na yale yaliyomtokea  basi kilichofuata ni KUSUSIWA NA KUTAKA UKOO WAKE(BANU HASHIIM) UMUONDOE MAKKA. BISMILLAH RAHMAN RAHIIM. Naam na baada ya Makureishi kushindwa kumnyamazisha Mtume Muhammad kwa Vituko,Rushwa na Mateso basi waliamua  Ukoo wake wa Banu Hashiim umuondoe MAKKA lakini Banu Hashiim walikataa. Baada ya hapo Mkaureishi waliwaamrisha Mtume Muhammad, Wafuasi wake na Ukoo wa Banu Hashiim watoke Makka na kwenda kuishi kwenye Mlima uitwao.Shuab Abu talib,Banu hashiim waliama Makka na kwenda kuishi huko kwa Miaka (3) huku wak...

Historia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi :4

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan,naam hakika kwa Rehma za Allah(S.W) ni siku nyingine tena tunakutana kujuzana machache kuhusiana na Historiya ya Mtume Muhammad(S.A.W). Naam na leo tutaangalia ni vipi Mtume Muhammad alianza kutangaza DINI kwa wasio waislamu. Mtume Muhammad alianza kutangaza DINI YA UISLAM YA ALLAH kwa wasio waislaam polepole na kwa siri kwa marafiki na jamaa zake kwa muda wa miaka(3) na watu waliosilim ndani ya mda huu walikuwa chini ya Thalathini. Baadhi ya watu waliosilimu ndani ya muda huu ni. Bi Khadija (R.A) Ali (K.W)Binamu na mtoto wa kumlea wa Mtume Muhammad(S.A.W). Zaiid,Mtumwa aliyeachiwa huru na Muhammad. Abu Bakar Sadiq(R.A) Uthman Ibin Affan(R.A) Talha. Hawa walikuwa watu wa karibu na marafiki wakubwa wa Mtume Muhammad(S.A.W) Na baada ya miaka (3) hii ya kutangaza DINI ya ALLAH hapo ndipo ALLAH akamuamrisha Mtume wetu Kipenzi wa Darja aanze kutangaza DINI waziwazi bila kificho. Na hapa sasa Mtume Mu...

Histotia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi :3.

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan,nirudie tena kuomba samahan kwa watumiaji wa blog hii na kwa kuwa nachukua mda mrefu bila kupost taarifa kwa kuwa bado niko Chuo basi In Sha ALLAH tusameheane na Allah hatusamehe pia.Na kwa hakika kwa leo hii tutaendelea kujuzana Historiya ya Mtume wetu Muhammad sehem ya 3 kwa ufupi kwa kile nilichoja'aliwa kukijua.KAREEBUN. SIFA ZA MTUME MUHAMMAD(S.A.W) Alikuwa mweye kusamehe kwa waliomkosea na Mrehemevu. Hakuwai kuabudu Masanamu wala kufanya Ushirikina. Alitumia pango la Hira, Mlima karibu na Makka kwa kutamalaki na kutafakari kuhusu jamii yake. Muhammad alikuwa akijulikana kwa tabia zake njeman na heshima. Watu walimwita (Al Amiin)yaani ni mwenye kuamini/muaminifu. Hizi ni baadhi ya sifa za Mtume wetu Kipenzi na ziko nyingi zaidi ya hizi. MUHAMMMAD NI MTUME WA MWENYEZI MUNGU(ALLAH).  Muhammad alikuwa anatumia pango la Hira kutamalaki na kutafakari juu ya Muambile ya Dunia na vilivyomo ndani ...

Historia ya Mtume Muhammad(S.A.W) kwa Ufupi:2

Aslaam 'Alaykum wa Rahmatullah wa Barakatuh ndugu zangu katika Iymaan,kwanza naomba mnisamehe kwa kuwa nakaa kimya mda mrefu bila kuweka kitu chochote kwenye blog yetu,naam na leo In Sha Allah tuendelee na Historia ya Mtume wetu Muhammad(S.A.W). Na leo tutangaanglia wake wa Mtume Muhammad  kwa kile nilichoja'aliwa kukifahamu ndugu yenu. Mtume Muhammad ndoa yake ya kwanza ilikuwa wakati yeye akiwa na miaka 25 na akamuoa mwanamke mmoja kati ya wale waliotabiriwa pepo Bi KHADIJA(R.A) na wakati huu bi Khadija alikuwa na miaka 40. Na hapa Bi Khadija ndiye aliyetokuwa wa kwanza kumwambia Mtume Muhammad kuwa anahitaji amuoe na hii ilitokana na sifa njema alizonazo na ufanyaji biashara wa Mtume Muhammad  (S.A.W) ambao ulikuwa na faida kubwa sana ambayo haikuwa na Riba ndani yake pia ni kutokana na Bi Khadija kuwa Mjane.Na ninachkumbuka ni kuwa Mtume Muhammad alikuwa kijakazi na baadae akawa anamfanyia biashara Bi Khadija japo sina hakika sana Allah anajua zaidi.Hivyo basi ndoa yao...